Search This Blog

Tuesday, November 9, 2010

KIKOSI CHA KILIMANJARO STARS KWA AJILI YA TASKER CUP HIKI HAPA


Kocha mkuu wa timu ya Taifa,Jan Poulsen akitangaza kikosi ya timu ya Kilimanjaro Stars leo katika ukumbi wa mikutano wa shirikisho la soka nchini (TFF).Wachezaji waliotajwa na kocha ni Akitangaza kikosi hicho kocha mkuu wa timu ya taifa Jean Paulsen amewataja wachezaji Juma Kaseja wa Simba, Shaban Kado na Said Muhando ambao ni magolikipa.Amewataja wachezaji wengine kuwa ni Shadrack Nsajigwa, Erasto Nyoni, Stephano Mwasyika, Haruna Shamte, Idrisa Rajab na Juma Nyoso ambao ni mabeki.
Viungo ni Shaaban Nditi, Henry Joseph, Nurdin Bakari, Jabir Azizi, Nizar Khalfan, Meshack Abel, Mohamed Banka na Kigi Makasi.Amewataja washabuliaji kuwa ni Danny Mrwanda,Mrisho Ngasa, John Bocco, Thomas Ulimwengu, na Mshabuliaji Gaudence Mwaikimba.Kikosi hicho ndicho kitakacho shiriki katika mashindano ya Cecafa Tusker Cup yanayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Novemba 27 mpaka Desemba 10,2010.katikati ni Meneja wa bia ya Tusker,Nandi Mwiyombella na kushoto ni Afisa Uhusiano wa SBL,Imani Lwinga

No comments:

Post a Comment