Search This Blog

Monday, November 8, 2010

CHENGE KUGOMBEA USPIKA!! Aaaaaah!!!

Pichani Mh.Andrew Chenge Mbunge wa Jimbo la Bariadi Mashariki na Mwanasheria mkuu wa Zamani wa Tanzania akiongea na waandishi wa habari kwenye hoteli ya Protea Courtyard Upanga SeaView leo ambapo amesema ana nia ya kugombea Uspika wa Bunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Amesema ameamua kugombea Uspika wa ili aweze kusimamia na kutibu majeraha ambayo yamesababishwa na uongozi uliopita kwa wengine.

Mswali ya kujiuliza ni haya:
1. Chenge ana kesi ya kifisadi Mahakamani, atawezaje kutibu majeraha ya kiutendaji wakati yeye ni mahututi?
2. Chenge ana kesi ya mauaji ya raia kwa kugonga na gari, je atawezaje kuwatetea walioathirika bungeni wakati ameshindwa kuwasaidia ndugu na jamaa wa wale aliwaua?



No comments:

Post a Comment