Search This Blog

Sunday, November 28, 2010

KIKWETE KUMWAMBIA DR. BILALI AKAFUNDISHE UDOM!!! IMEKAAJE???

Nimemsikia juzi Rais Kikwete akimwagiza Dr Bilal awe anaenda kutoa lecture pale UDOM. Kuna mambo ambayo wananchi ni bora tujiulize.  

1. Kufundisha chuo kikuu ni lazima taratibu zitumike, kwa mfano lazima awe mwajiriwa iwe full time au part time na lazima atasimamiwa kwamba kweli anafanya kazi hiyo na hatimaye atalipwa kwa kazi hiyo. Unadhani kama makamu wa rais ataweza kukidhi matakwa ya kazi hiyo? 

2. Inamaana tuamini kuwa U-Makamu wa Rais hauna majukumu makubwa kiasi cha kumruhusu mhusika kuendelea na majukumu mengine na tuamini kuwa U-Makamu wa Rais ni kazi rahisi saaaaaaaaaana!!!


3. Dr. Bilal kama Makamu wa Rais anapewa ulinzi na ndiyo maana anaandamana na walinzi muda wote katika majukumu yake. Je, atakuwa anaingia nao kwenye vyumba vya kufundishia? Au nje ya darasa ni lazima kuwe na askari wa kutosha kumlinda??, Je wanafunzi wote wafanyiwe screening kabla ya kuingia kwenye kipindi au kama walikuwepo watoke wawe screened then waingie, kipindi si kitakuwa kimeisha kabla ya kuanza jamani!!!??. Na hizo kelele za ving'ora kila siku si itakuwa kero?? 

Kauli za JK huwa zinabeba maana anayoijua yeye. Mbona Shein ni Dr lakini haikuwahi kutokea kuambiwa akashike chaki kufundisha?. Hii itakuwa ni zaidi ya udhalilishaji na ni tatizo la JK kutokuzingatia hotuba ndio maana anajikuta kila siku yuko off-point.

Nadhani washauri wake wawe makini ila tuna mshukuru kwa kutufahamisha kuwa Makamu wa Rais hana kazi kubwa za cheo hicho hata kama atakaa Dodoma kuendelea kufundisha mambo pale Ikulu yataendelea tu.

Nawasilishaaaaaaaa!

No comments:

Post a Comment