Search This Blog

Monday, November 22, 2010

SITASHANGAA HAYA KUTOKEA TANZANIA


Mimi sitashangaa yafuatayo kutokea:

Sitashangaa wananchi washabiki wa CCM kusikitishwa na uteuzi wa nafasi mbalimbali utakaofanywa na JK... utasikia wanasema du kawaweka maswahiba wake.
Sitashangaa wananchi washabiki wa CCM kulalamikia rushwa kushamiri Tanzania .. kama kwamba walikosa mbadala wa kumweka uongozini kupambana na rushwa kwa umakini zaidi ..
Sitashangaa wananchi mashabiki wa CCM kuanza kulalamikia hali ngumu ya maisha.. ngoja nitoe scenario moja: Chadema wana sera ya elimu bure hadi kidato cha sita (6) kama si chuo kikuu. lakini sitashangaa walioinyima kura Chadema kuanza kuja kwako kukupigia magoti kuomba msaada wa kifedha ili apate ada ya kumpeleka mtoto sekondari. Wakati walikataa kuichagua iondoe hiyo kero. Sitashangaa elimu ya namna hii ikiendelea kutolewa na CCM huku wanachi wakishangilia ati CCM oyeeeeee!!

Sitashangaa wananchi washabiki wa CCM waliokuwa wanavaa sare na kucheza kama hawana akili nzuri wakati wa mikutano ya kampeni kuendelea kuwa katika hali zao duni............ why? kwa sababu serikali imeshindwa kuwa na dira endelevu.
Sitashangaa wananchi mashabiki wa CCM kuendelea kuishi katika nyumba za mbavu za mbwa  wakati wamekataa kumpigia kura Dr. Slaa aliyekuwa ameahidi kushusha bei ya saruji (cement) ili wananchi walio wengi waweze kujenga nyumba imara na bora

Sitashangaa wanachi mashabiki wa CCM kuendelea kulalamikia ukosefu wa dawa hospitalini..
Sitashangaa wananchi na mashabiki wa CCM kuendelea kulalamikia utendaji mbovu wa idara mbalimbali za serikali (kumbuka jinsi Clouds walivyokuwa wanachambua utendaji mbovu wa idara mbalimbali e.g. EWURA, DAWASCO, TANESCO lakini wakawa vuvuzela wa CCM wakati wa uchaguzi)
Sitashangaa wapenzi wa CCM kulalamikia mishahara wanayopata na wakati huo huo kulalamikia posho kubwa za viongozi wakati wao maisha ni magumu hata kushindwa kuendesha biashara zao na kuinua kipato

Sitashangaa watu hawa kuvaa ma- Tshirt, kofia na kanga 2015 kushangilia na kushabikia CCM wakati wa uchaguzi mwingine.

Kutokana na hili naomba tushirikiane pamoja kuzidi kutoa elimu ya uraia, ipo siku yatabadilika ... "MAFISADI YANA MWISHO" Dr Slaa.

No comments:

Post a Comment