Search This Blog

Friday, November 5, 2010

HAYA NDIYO MATOKEO YA MWISHO YA URAIS YALIYOTANGAZWA NA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI



MATOKEO RASMI YALIYOTANGAZWA LEO
1. KUGA PETER MZIRAY APPT - MAENDELEO: 96, 933 (1.12%)

2. KIKWETE JAKAYA MRISHO/CCM: 5,276,827 (61.17%)

3. SLAA WILLIBROD PETER/CHADEMA: 2,271,941 (26.34%)

4. LIPUMBA IBRAHIM HARUNA/CUF: 695,667 (8.067%)

5. RUNGWE HASHIM SPUNDA/NCCR-MAGEUZI: 26,388 (0.31%)

6. MGAYWA MUTTAMWEGA BHATT/TLP:17,482 (0.20%) 
7. DOVUTWA YAHMI NASSORO DOVUTWA/UPDP: 13,176 (0.15%)
----------------------------------------------
WALIOJIANDIKISHA KUPIGA KURA: 20, 137, 303
WALIOJITOKEZA KUPIGA KURA: 8, 626 (42.64%)
KULA HALALI ZILIZOPIGWA: 8,398,394
KURA ZILIZOHARIBIKA 227,889 (2.64)

MWENYEKITI wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, ( NEC), Jaji Mstaafu, Lewis Makame leo jioni amemtangaza mshindi wa kiti cha urais wa Tanzania wa mwaka 2010 kuwa ni Ndugu Jakaya Kikwete kutoka Chama cha Mapinduzi(CCM).

Matokeo hayo ya uchaguzi huo, yalitangazwa leo majira ya saa kumi jioni na Mwenyekiti huyo katika viwanja wa Karimjee jijini Dar es Salaam.

Kabla ya kutangazwa kwa matokeo hayo, Jaji Mstaafu , Makame alisema kwa mujibu wa Ibara ya 41(6) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mwaka 1977 mgombea wa kiti cha urais atatangazwa kuwa amechaguliwa kuwa rais iwapo tu amepata kura nyingi kuliko mgombea mwingine yeyote.

Aidha Makame alisema kwa mujibu wa ibara ya 47(2) ya Katiba hiyo, mgombea wa kiti cha urais akichaguliwa basin a mgombea mwenza wake atakuwa Makamu wa Rais.

No comments:

Post a Comment