Search This Blog

Sunday, February 20, 2011

MAAMUZI YA JK NA BARAZA LA USALAMA LA TAIFA HAYA HAPA:


TUMETOA BAADHI TU YA MAAMUZI YA BARAZA LA USALAMA LA TAIFA.......


5. Aidha, Kamati ya Maafa ya Mkoa imeelekezwa kutengeneza taratibu nzuri zitakazohakikisha kuwa mapema iwezekanavyo, wananchi hao wanarejea makwao ili waendelee na shughuli zao za kawaida hasa sasa ambapo hatari ya milipuko katika maghala ya Gongolamboto haipo tena.
JAMANI HEBU ANGALIA HIYO PICHA. JE KUNA UWEZEKANO WA MTU KURUDI KUISHI HUMO NA KUENDELEA NA SHUGHULI ZAKE??? SOMA NAMBA 5 HAPO JUU. NILIDHANI BARAZA LINGEAMUA KUWEPO NA UTARATIBU WA KUTOA MAHEMA (TENTS) KWA WAATHIRIKA, AMA KUWAPELEKA KATIKA BAADHI YA NYUMBA ZA SERIKALI KWA MUDA. MAANA MIUNDOMBINU IMEHARIBIKA SANA. HUWEZI KUENDELEA NA SHUGHULI WAKATI NYUMBA HAIPO NI MAJIVU TU. HAWA JAMAA VIPI??

2. Kuhusu waliopoteza maisha, tumeamua kuwa, Serikali igharamie mazishi ya marehemu wetu hao popote ndugu watakapoamua wakazikwe. Baadae ndugu wa marehemu wapewe kifuta machozi.
WASIWASI WETU NI KUWA HADI MUDA HUU TAKWIMU SAHIHI ZINATIA UTATA MAANA INASEMEKAMA WALIOFARIKI NI WENGI. TUKIO LA MBAGALA HADI SASA MALIPO HAYAJAKAMILIKA, IWEJE LA GONGOLAMBOTO?? WAWAJIBIKE!!!!

8. Baraza la Usalama la Taifa, limeagiza Kamati ya Maafa ya Mkoa wa Dar es Salaam na Kitengo cha Maafa cha Taifa wazitambue mapema iwezekanavyo nyumba zilizoharibiwa, wenye nyumba na kuhakikisha kuwa matayarisho husika yanafanyika ikiwa ni pamoja na uthamini ili walipwe fidia wanayostahili bila kuchelewa.
TUNAOMBA KAMATI HII IANGALIWE UPYA MAANA MBAGALA WALIPROVE FAILURE.
14. Mwisho, Baraza la Usalama wa Taifa linawaomba wananchi waliohama warejee kwenye makazo yao kwani kipindi cha hatari ya mabomu kulipuka kimekwishapita. Tunaomba na kusisitiza wajiepushe kuchezea mabomu yaliyodondoka katika maeneo yao ambayo bado hayajaondolewa
KIPINDI CHA HATARI BADO HAKIJAPITA MAANA MABOMU NDO HASA YAPO URAIANI AMBAPO JK NA BARAZA LA USALAMA LA TAIFA LINAWATAKA WANANCHI WAKAISHI NAYO HUKO AMBAPO MABOMU YAMEDONDOKA. JE NI NAMNA GANI UTAWAZUIA MIFUGO INAYOCHUNGA MAENEO YA WAZI WASIYAGUSE HAYO MABOMU??? NADHANI KWA KIPINDI HIKI SERIKALI INGEWAHIFADHI WANANCHI SEHEMU SALAMA ZAIDI MAANA MABOMU YAMESAMBAA GONGOLAMBOTO NA MAENEO YA JIRANI.
KUNA DALILI YA HUZUNI HAPO?????




No comments:

Post a Comment