Search This Blog

Friday, February 25, 2011

TAARIFA YA MSIBA

Ukoo wa Mukama, wa Majita  Musoma, wanasikitika kutangaza kifo cha Ndugu yetu mpendwa Japhet Muura Mukama kilichotokea jana 24/2/2011 hospitali ya Muhimbili. Mazishi yatafanyika Jumapili tarehe 27/2/2011 Dar es Salaam. Marehemu ameacha Mke na watoto watano - Joyce, Mukama, Mercy,Kabuche na Kainda. Mwana blog hii (Baraka Mukama) ni miongoni mwa wadogo zake na marehemu. Tunaomba sana kwa kipindi hiki cha masikitiko na majonzi Bwana Mungu awe pamoja nasi. Atupe faraja ya pekee na sisi tuliobaki tuwe na umoja, amani na upendo. Tunashukuru kwa wote waliotutumia salaamu za rambirambi.
Bwana alitoa na Bwana alitwaa jina na Bwana libarikiwe. Amen

No comments:

Post a Comment