Search This Blog

Friday, January 21, 2011

IKO WAPI INTELIJENSIA YA POLISI??


MFUMO wa Polisi, vyombo vingine vya ulinzi na usalama na serikali,wa kukusanyia na kusafirishia taarifa, hasa za “usalama,” ujulikanao kama intelijensia una walakini.
Said Mwema, inspekta jenerali wa polisi (IGP), alisema alikuwa na “taarifa za kiintelijensia” kuwa kutatokea vurugu iwapo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kitafanya maandamano mjini Arusha.
Iko wapi intelijensia ya polisi isiyoweza kuona Mafisadi na kuwakamata wanaounda makampuni na kuiba mabilioni ya shilingi kutoka Benki Kuu na Hazina?
Iko wapi Intelijensia ya IGP Mwema isiyoweza kujua mmiliki wa Dowans na ndugu yake Richmond? Kwa nini inteligensia ya Mwema isizuie malipo ya mabilioni ya shilingi kufidia kisichoeleweka wakati wahusika wapo?
Au hii Intelijensia ni kwa Chadema tu????????????????

No comments:

Post a Comment