Search This Blog

Thursday, February 17, 2011

BREAKING NEWS !!!! GONGOLAMBOTO YALIPULIWA NA MABOMU!!

Maeneo ya Gongolamboto Dar, yakilipuka na mabomu!!! Hali inatisha

Jiji zima la Dar maeneo mengi yalihathirika na mabomu

Majeruhi wakipata matibabu hospital ya Amama

Vijana na watoto walipata majeraha na wengine kupoteza maisha.

Watu kadhaa wamekufa kwa kupigwa na mabomu na kugongwa na magari baada ya kusikika kwa mlipuko wa mabomu maeneo ya Gongolamboto. Hali hadi muda huu inasikitisha sana. HIVI KWA NINI SERIKALI ISIWAJIBIKE??

Maeneo mengi yaliyopo ndani ya mji wa Dar es salaam inashangaza kumilikiwa na Jeshi la Wananchi mfano:Kigamboni(mwanzoni)i,Masaki,Mwenge (Lugalo),Mikocheni,Msasani,Kawe n.k haya ni maeneo yalipaswa kuwa makazi rasmi ya Wananchi. Tofauti yake ni kuwa Wananchi wanaishi nje ya Mji na jeshi linamiliki katikati maeneo ya jiji la DSM huku maeneo yake mengi yakiwa wazi eti mara Range,mara mess.Hili jeshi la ajabu huwezi kulinda Wananchi ukiwa katikati yao,hapo ni kuwa jeshi ndilo linalindwa na Wananchi. Kutokana na ukuaji wa Mji,na kwa usalama wa raia na shughuli za kijeshi na kazi zao Wanajeshi walipaswa KUHAMA na kuelekea nje ya Mji. Mbona Tanzania tumebahatika kuwa na maeneo mengi tu ya wazi nje ya miji. Kwa nini jeshi linang'ang'ania kuishi na mabomu yao mijini? Hii ni hatari.

Leo hii tunapoteza watu wengi kwa uzembe wa serikali,kusababisha ulemavu wa Maisha na kuongeza umasikini, kupoteza rasilimali kidogo za wananchi kwa uzembe usiohitaji usiohitaji hata kuunda tume. Serikali mara ngapi itatoa fidia na kutumia gharama nyingi za kimaafa.

Ebu tuache "SIASA" ni wakati sasa kwa JWTZ kuhama maeneo ya Raia na kuelekea nje kabisa ya mji,huko mtakuwa mmetunusuru jamani.
BLOG HII INATOA POLE NA RAMBIRAMBI KWA WOTE WALIOATHIRIKA NA MABOMU YA GONGOLAMBOTO. 




No comments:

Post a Comment