Search This Blog

Friday, April 1, 2011

TANZANIA YAWEKA REKODI YA NOTI.....kati ya noti hizo hapo chini ni ipi noti mpya?

Kwa mara ya kwanza Tanzania imeweka rekodi ya pesa/Noti kama ifuatavyo:
1. Kuwepo kwa noti mbili (2) zenye kiwango sawa na zipo katika mzunguko kwa wakati mmoja na kwa muda mrefu sasa.
2. Noti mpya inazeeka na kuchakaa mapema kuliko noti ya zamani. Ukiangalia picha hiyo hapo juu utadhani noti ya upande wa chini ndio ya zamani,, kumbe ni mpyaaaaaa ina umri wa miezi minne(4) tu.

Sielewi kwa nini BoT inapata kigugumizi kushughulikia tatizo la hizo noti ambazo wanaziita mpya na zinatoa rangi kama batiki......kumbe hamna lolote!! Jamani serikali hii imeshindwa kabisa kuwajibika maana ni maajabu sana noti ndani ya miezi minne tu noti imeshazeeka, je ikimaliza miaka 5 si tutabaki na sarafu tu?????
Nawasilisha.

No comments:

Post a Comment