Search This Blog

Friday, July 8, 2011

VURUGU ZA WAMACHINGA NA POLISI: chanzo chajulikana........

Vurugu za wamachinga na mgambo zilizotokea juzi jijini hapa, zimedaiwa kusababishwa na mvutano baina ya ofisi ya Meya na Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza.

Madai hayo yalitolewa jana na Meya wa Jiji, Josephat Manyerere (Chadema), wakati akizungumza wa waandishi wa habari ambapo alidai kwamba ofisi yake haikupewa taarifa ya operesheni ya kuondoa wamachinga katika maeneo yasiyoruhusiwa kufanya biashara katika mtaa wa Makoroboi.

Alipofuatilia, alibaini kuwa hata ofisi ya Mbunge wa Nyamagana, haikuwa na taarifa ya operesheni hiyo, ambayo imesababisha watu saba kujeruhiwa na kwamba habari zilizoenezwa kuwa Chadema walihusika na vurugu hizo kwa sababu halmashauri
inayoongozwa na chama hicho ni ya uchochezi.


 Amesema kwa kuwa operesheni hiyo ni batili, amewataka wamachinga waendelee kufanya biashara katika maeneo ya Makoroboi, hadi suala lao litakapopelekwa kwenye Baraza la Madiwani, ili kutafutiwa utaratibu na maeneo yasiyo na bughudha. Mvutano huo wa kiuhusiano, umesababisha ofisi ya Mkurugenzi kutotoa ushirikiano kwa ofisi ya Meya na kutolea mfano wa uuzwaji wa viwanja katika eneo la Kiseke bila ofisi yake kujulishwa.

Aidha, ametoa wito kwa wamachinga kujitahidi kupanga bidhaa zao vizuri, ili watu wapate njia ya kupita na pia wasitumie vipaza sauti kutangaza bidhaa zao na kuhakikisha maeneo ya biashara yanabaki safi na wafanye biashara hizo kuanzia saa 10 jioni.

Amewaomba wenye misikiti na shule katika mtaa wa Makoroboi waendelee kuwavumilia hadi ufumbuzi wa kudumu utakapopatikana kutokana na kwamba kulegalega kwa uhusiano wa kikazi kumesababisha vurugu zilizotokea juzi.

No comments:

Post a Comment