Search This Blog

Monday, July 11, 2011

UONGOZI MBOVU NDO UMESABABISHA HAYA:

Idadi ya vijana wasiokuwa na ajira inazidi kuongezeka, elimu katika mashule yetu inazidi kushuka. Huduma katika hospitali zetu na katika vituo vya afya ni mbaya kiasi cha watu kutumia mitishamba.
Sote tunajua kuwa maeneo mengi hapa nchini hawana chakula na watu wanaishi kwa mlo mmoja tu kwa siku, bei ya vyakula sokoni imepanda na thamani ya shilingi yetu imeshuka kuliko kipindi chochote kile tangu nchi hii ipate uhuru.

Uzalishaji viwandani umeshuka, na hakuna shirika la umma linalifanya vizuri, hakuna hata ndege kubwa ya serikali inayoruka. Aibu kubwa hii!!!
Kilimo kwanza ni wimbo uliotungwa, lakini hauna mchezaji wa wimbo huo. Hakuna ongezeko la mazao ya chakula na biashara ukiuliza unaambiwa ni ukame. Hivi wakati wanatunga huo wimbo hawakujua kuna ukame???

Giza!!!! Jamani Giza!!! Ni miaka takribani 50 ya uhuru wan chi hii nchi ni giza kila siku kwa mgao usioisha. Wakati huo viongozi wanazunguka duniani kutafuta wawekezaji. Je wawekezaji watawekeza gizani?
Kuna watanzania wameiba pesa za wananchi! Mafisadi wanatanua tu mitaani kama mabingwa wa ligi Fulani. Ukiuliza unajibiwa hakuna ushahidi wa kuwatia hatiani
Askari polisi kuuwa raia wasio na hatia imekuwa ni jambo la kawaida. Wamachinga wamepigwa risasi Mwanza lakini ikaonekana uchunguzi utafuata!! Wapi nyie mnaua watu?

No comments:

Post a Comment