Search This Blog

Monday, July 18, 2011

WABUNGE WAKATAA UTITIRI WA MIPANGO YA NGEREJA!!!

Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini imekwama kupita na kusogezwa mbele kwa muda wa wiki tatu ili  kutoa majibu muafaka kuhusu mgao wa umeme pamoja na mambo mangine.
Hoja ya kuhairisha bajeti hiyo imetolewa na Kiongozi wa Serikali Bungeni Waziri mkuu Mizengo Pinda, bunge bila kujari itikadi za vyama limepitisha kwa kauli moja hoja hiyo.Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini mwaka 2011/12, ilikuwa mbaya na mbovu isiyofaa hata kupitishwa kwa kutoridhishwa na mipango iliyomo katika bajeti.Miradi 16 iliyohitaji Sh402.4 bilioni ikiwa ni pamoja na matumizi ya kawaida ni:-
1.     Mitambo ya kufua umeme ya megawati 100 jijini Dar es Salaam utakamilika Desemba mwaka huu
2.     Megawati 60 jijini Mwanza ambao utakamilika Juni mwakani.
3.     Kinyerezi (Dar es Salaam) wa megawati 240 (utakamilika mwaka 2013/14),
4.     Mnazi Bay (Mtwara) wa megawati 300 (utakamilika mwaka 2013/14),
5.     Somanga Fungu (Kilwa), megawati 230 (utakamilika mwaka 2013/14)
6.     Ruhudji, megawati 358 (utakamilika mwaka 2015/16).
7.     Mgodi wa makaa ya mawe Kiwira (Mbeya) megawati 200 (utakamilika mwaka 2013/14),
8.     Ngaka wa megawati 400 (utakamilika mwaka 2014/15),
9.     Mchuchuma megawati 600 (utakamilika mwaka 2014/15),
10.  Murongo/Kikagati (Kagerea) wa megawati 16 ambao utategemea kukamilika kwa makubaliano kati ya Serikali ya Uganda na Tanzania.
11.  Rusumo (Kagera) wa megawati 63 ambao upo kwenye taratibu za kutafutiwa fedha,
12.  Stiegler's Gorge (Pwani) wa megawati 2,100
13.  Mpanga wa megawati 165 (utakamilika mwaka 2015/16).
14.  Rumakali wa megawati 222 (utakamilika mwaka 2018),
15.  Dar es Salaam-Tanga ambayo ni ya dharura ikijumuiasha Symbion (megawati 112.5), Aggreko (megawati 100),
16.  Ununuzi wa mitambo itakayofungwa Majani Mapana, Tanga wa megawati 70 na ule wa gesi wa IPTL, Tegeta jijini Dar es Salaam.
Hebu tusubiri watakuja na mipango gani tena baada ya hizo wiki tatu!!!!

No comments:

Post a Comment