Search This Blog

Sunday, April 10, 2011

BREAKING NEWS !!!! MUKAMA KATIBU MKUU CCM, Makamba na unabii wake chali

Katibu Mkuu mpya CCM (kulia) Bw. Wilson Mukama


Nape Nauye "Uenezi unaanzia hapa hapa"
 Habari tulizopokea ni kwamba, hatimaye, CCM imeamua kumpiga kibuti katibu wake Mkuu Yusuf Makamba. Nafasi yake imechukuliwa na aliyewahi kuwa mkurugenzi wa jiji la Dar Es Salaam, Wilson Mukama.  Naye Nape Nnauye amechukua nafasi ya itikadi na uenezi ilikuwa ikishikiliwa na John Chiligati. Inaonekana zamu hii ni ya watoto wa wakongwe wa CCM. Maana Rehema Nchimbi mtoto wa John Nchimbi baba yake Emanuel Nchimbi,kama Nape, amechukua nafasi ya katibu wa organizesheni.

Swahiba mwingine wa Kikwete, Zakhia Meghji aliyetupwa nje kwa kashfa ya EPA benki kuu na anayedaiwa kushiriki ufisadi wa kutisha kwenye wizara ya utalii amerejea kwa kishindo kwa kunyakua nafasi ya katibu wa fedha na uchumi iliyokuwa chini ya Amos Makala.

Wachambuzi wa mambo wanasema kuwa CCM imeamua kujivua gamba kwa kuwatimua vinara na watetezi wa ufisadi hasa Makamba. Hatimaye Kikwete amelitupa jini na jinamizi la Makamba ambaye kimsingi alikuwa akimtawala Kikwete pamoja na uenyekiti wake. Bila shaka akina Tambwe Hiza sasa wanajinonihii kwenye suruali kutokana na muungu wao Makamba kupigwa buti. Je imejivua gamba au ni gamba lile lile la kujuana, kulindana, kufisidi, kuganga njaa, usanii na upuuzi mwingine? Time will tell.

......sijui nitoroke hata hiki kikao!!!! watu hawa hawana hata huruma- Makamba naye katimuliwa U-katibu mkuu aliyejifanya Nabii ndani ya CCM iliyooza.
"Poa tu"--Makala -  .......Ndo wale wale waliokunywa uji wa mgonjwa

No comments:

Post a Comment