Search This Blog

Friday, October 7, 2011

Kwa matokeo ya Igunga tutegemee "VUA GAMBA PART 2"

Pamoja na maneno mengi ya kuonyesha kuwa kuna umakini na mvuto wa kisiasa katika jamii, lakini kwa watu wanaojua kutafakari na kupambanua mabo ni dhahiri kuwa Chadema imeweza kuleta mabadiriko ya kisiasa Tanzania. 

Ebu turejee matokeo ya Igunga kidogo:
Mwaka 2010 CCM walipata kura 36,000: Uchaguzi mdogo wa juzi wakaambulia kura 26,484 ambazo zimepatikana katika mazingira yanayolalamikiwa na wadau wa maendeleo ya kijamii.
Mwaka 2010 CHADEMA hawakupata kura: Uchaguzi mdogo wakapata kura 23,286 hii inaonekana wamepanda chati na kukubalika katika jamii.
Mwaka 2010 CUF walipata kura 11,000: Uchaguzi mdogo wakaambulia kura 2,014.

Hebu tutafakari haya:
Je kwa takwimu hizo ni chama gani chenye mvuto katika jamii??Kutokana na mwenendo wa kisiasa?

Tukirejea kwenye gharama zilizotumika, CCM ilitumia Tshs 3biln, CHADEMA Tshs 400Mln na CUF Tshs 150Mln. CCM wamepata kura 26,484, CHADEMA kura 23,286, CUF kura 2,104, kwa hesabu za haraka ukigawanya idadi ya pesa na kura walizopata hali itakuwa hii: CCM:3,000,000,000/26,484=113,275/=
CHADEMA:400,000,000/23,286=17177/=
CUF:150,000,000/2,104=71,292/= hivyo basi
CCM imetumia Tsh 113,275/= kupata kura moja.
CDM imetumia Tsh 17,177/= kupata kura moja
CUF imetumia Tsh 71,292/= kupata kura moja
Kwa uchambuzi huo utaona kuwa CHADEMA inakubalika kwa jamii bila hata ya kutumia gharama kubwa ya kipesa. Ikiwa na maana kuwa sera na hoja zinakubalika zaidi kwa jamii na kimeleta imani katika jamii zaidi kuliko wale wanaotumia hela nyingi kutafuta imani na umaaufu kwa jamii. Kwa hiyo CCM walitumia pesa nyingi sana kutafuta kura moja uliko vyama vingine na hii inaonyesha kuwa imepoteza imani kwa jamii ndo maana inawagharimu kupata idadi ya kura.

Ukiona chama chako kinaporomoka kwa idadi ya kura basi sioni sababu ya kushangilia eti umeshinda kwa kishindo wakati kila kukicha wananchi wako wanakuchoka. Chama chenye takwimu ambayo inapanda kila siku kinadhiirisha kuwa wapo focused na kina uongozi madhubuti na kinakubalika kwa wananchi. 

Nadhani ile falsafa ya kujivua gamba tafakari yake siyo kwa viongozi tu ila hata wanachama wake nao wanajivua gamba na ku-support chama kingine kilicho na msimamo makini. Nadhani kwa matokeo ya Igunga tutegemee "vua gamba part 2" baada ya part 1 kuonekana imewashindwa.

Mungu ibariki Tanzania


Tuesday, September 27, 2011

JE HII NDIYO TANZANIA TUNAYOITAKA WAKATI WA UCHAGUZI??

CCM ndo wanaoongoza kwa ushawishi wa vurugu maeneo mengi kama Igunga kwa kuwatisha wananchi ili ichaguliwe. Je ndiyo Tanzania tunayosikia ni nchi ya amani? Kama ni amani mbona Viongozi kama huyu Aden Rage anapiga kampeni akiwa na bastola kiunoni. Nijuavyo mimi kila mikutano ya adhara huwa kuna askari wa kulinda usalama. Inakuwaje silaha hadharani hivyo???

Thursday, September 15, 2011

HAMA HAMA YA WAKUU WA MIKOA TZ

Na. JINA LA MKUU WA MKOA KITUO AENDAKO KITUO ATOKAKO
1. Bw. Saidi Mecki Sadiki DAR ES SALAAM RC - Lindi
2. Bw. John Gabriel Tupa MARA DC - Dodoma
3. Bw. Saidi Thabit Mwambungu RUVUMA DC - Morogoro
4. Kanali Joseph Simbakalia MTWARA RC Kigoma
5. Bi. Chiku S. Gallawa TANGA DC - Temeke
6. Bw. Abbas Kandoro MBEYA RC Mwanza
7. Bw. Leonidas T. Gama KILIMANJARO DC – Ilala
8. Dkt. Parseko Ole Kone SINGIDA RC Singida
9. Eng. Stella Manyanya RUKWA Mbunge V/Maalum
10. Bibi Christine Ishengoma IRINGA RC Ruvuma
11. Dk. Rehema Nchimbi DODOMA DC - Newala
12. Bw. Elaston John Mbwillo MANYARA DC – Mtwara
13. Col. Fabian I. Massawe KAGERA DC - Karagwe
14. Bibi. Mwantumu Mahiza PWANI Mbunge/NW Mstaafu
15. Bibi. Fatma A. Mwassa TABORA DC - Mvomero
16. Bw. Ali Nassoro Rufunga LINDI DC - Manyoni
17. Eng. Ernest Welle Ndikillo MWANZA DC - Kilombero
18. Lt. Col. Issa Machibya KIGOMA RC Morogoro
19. Bw. Magesa S. Mulongo ARUSHA DC - Bagamoyo
20. Bw. Joel Nkaya Bendera MOROGORO Mbunge/NW Mstaafu
21. Bw. Ludovick Mwananzila SHINYANGA Mbunge/NW Mstaafu


Miaka 50 ya Uhuru: UKWELI NA UONGO!


Hivi ni kweli kabisa kuwa 09/12/2011 tunasherehekea miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania??Sasa hivi kila idara ya serikali, mashirika na taasisi zake zinafanya maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru.
Hebu tutafakari kwa akili huru kwa pamoja
1. Tanzania ilizaliwa mara baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kuungana tarehe 26/04/1964 ambako mpaka leo ni miaka 47 ya muungano kwa maana hiyo Tanzania ina miaka 47 na sio 50 kama tunavyorubuniwa nah ii serikali na kutumia fedha nyingi kutangaza eti miaka 50 ya uhuru wa Tanzania
2. Kwanini Serikali isiseme tunasherehekea miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika au Tanzania Bara badala ya kuendelea kusema Tanzania?? Na kama dhana ni miaka 50 ya uhuru basi ni UHURU wa TANGANYIKA na siyo Tanzania.
3. Siku ya sherehe ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania kama wanavyosema wimbo gani wa Taifa utaimbwa?Mungu Ibariki ambao ni wimbo wa taifa Tanganyika na Zanzibar kwa Ujumla au utaimbwa uliokuwa wimbo wa Tanganyika? Au ule wa wasanii wa bongoflava??
4. Siku ya sherehe bendera gani itapeperushwa na kupandishwa?hii inayotumika sasa ikiashiria Muungano wa Tanganyika na Zanzibar au ile ya Tanganyika ambayo daima mzee  Mtikila huipandisha?
5. Mgeni Rasmi atakuwa nani?Mhe Jakaya Kikwete ambae ni Rais wa jumla wa Tanzania bara na Zanzibar?
Imefika wakati wa kuwa na Bendera ya Tanganyika kama ilivyo Zanzibar, Jina la Tanganyika likaendelea kuwepo na kutambulika kama lilivyo la Zanzibar, Heri tukawa na Wimbo wa Taifa la Tanganyika kama ilivyokuwa zanzibar
Mbona Zanzibar wakisherehekea miaka yao mapinduzi huwa wanapandisha bendera yao?mbona wao wana imba nyimbo za kusifu mapinduzi na wimbo wa taifa lao?
Nawasilisha!!!!!!!



Monday, September 12, 2011

Katuni ya leo

CCM wameanza kwa kuhonga wali Igunga

Hapa ni wali

Hapa wakisomba watu kuwapeleka mkutanoni??
Jamani waungwana.....Hii siyo rushwa???

Hisia za Mhe. Zitto Kabwe juu ya msiba huu wa kitaifa

Taifa Msibani, Umoja wetu na Utu wetu Shakani
by Zitto Z Kabwe on Sunday, 11 September 2011 at 16:19

(Nimeandika makala hii nikiwa katika Benchi la Hospitali ya Mnazi
 
Mmoja hapa Zanzibar. Mniwie radhi kama kuna spelling mistakes kwani
nilitaka hisia zangu ziwe as raw as possible - Zitto Zitto and not
Zitto a Politician).

Jana asubuhi tarehe 10 Septemba 2011 Taifa liligubikwa na habari za
 
kushtusha za maafa. Mwanzoni taarifa zilisambaa kwamba zaidi ya watu
2000 walikuwa kwenye Boti MV Spice Islander lililopinduka na kuzama
mbele kidogo ya Nungwi likielekea kisiwani Pemba. Habari hazikuwa za
uhakika sana kwani vyombo vyetu vya habari na hasa Televeshini ya
Taifa havikuwa vikitoa habari juu ya ajali hii.

Habari zilisambaa kupitia mitandao ya intaneti na kufuatia uchu wa
 
habari nilianzisha #ZanzibarBoatAccident katika mtandao wa twitter ili
tuweze kufuatilia kwa karibu habari zote za ajali hii.

Habari zilisambaa kuwa Televisheni ya Taifa ilikuwa inaonyesha muziki
 
wa Taarab na Baadaye vipindi vingine vya kawaida bila kutoa habari kwa
Umma kuhusu msiba huu.

Watanzania waliokoa wakiwasiliana kupitia twitter na facebook walikuwa
 
na hasira sana na kituo cha TBC1 kutoonyesha au kupasha habari juu ya
ajali hii. Mpaka saa moja jioni kituo hiki cha Televisheni ya Taifa
kilikuwa kinaonyesha watu wakicheza muziki wa Kongo, wanawake
wakikatika viuno na hata ngoma za asili.

'Hallo, washa TBC1 uone Televisheni yenu inachoonyesha' yalikuwa ni
 
maneno ya Mwakilishi Ismael Jussa Ladhu aliponipigia kuonyesha
kusikitishwa kwake na kituo hiki. Mpaka jioni tulikuwa tumepata
taarifa kuwa Watanzania wenzetu 198 walikuwa wamepoteza maisha. 570
hivi walikuwa wameokolewa.

Binafsi nilipotembelea Hospitali ya Mnazi Mmoja niliweza kumwona Binti
 
aliyeitwa Leyla, akisoma darasa la Nne huko kisiwani Pemba. Leyla
alipona, aliokolewa. Nilimwambia leyla atapona na kurudi Shuleni.
Mpaka ninapoandika tumeambiwa kuwa Watanzania 240 wamegundulika
kupoteza maisha na zaidi ya 600 wameokolewa.

Napenda kuwapongeza sana waokoaji wetu, wavuvi wa kijiji cha Nungwi na
 
vijiji jirani, wamiliki wa mahoteli waliojitolea vifaa vyao kwenda
kuokoa watu na wanajeshi wetu wa majeshi ya ulinzi na usalama kwa kazi
hii kubwa ya kuokoa. Kwa kweli tumeokoa watu wengi kuliko
ilivyotarajiwa. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imejitahidi sana,
ilitulia na kuonyesha uongozi thabiti katika juhudi za uokoaji.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akafuta ziara yake huko
 
Canada, ziara iliyokuwa imeandaliwa muda mrefu na kwa gharama. Lakini
Rais aliona ni vema kupata hasara kuliko kuwa nje ya Nchi kipindi
hiki. Hakutaka hata kumtuma Makamu wa Rais au Waziri Mkuu. Alifuta.
Akatangaza siku 3 za kuomboleza.

Hata hivyo waandaaji wa Miss Tanzania waliona hasara kubwa kuahirisha
 
shindano la Urembo usiku huo. Wangepata hasara! Hata wafadhili wao
Kampuni ya simu za mkononi ya vodacom ambao miongoni mwa waliofariki
wamo wateja wa vodacom, waliendelea na shindano hili.

Jumatatu, tarehe 12 Septemba 2011 ni siku ya khitma ya kuwaombea marehemu wetu.
 

Nimeamua kutotumia simu yangu ya Voda kwa siku nzima, sina njia ya
 
kuiadhibu Kampuni hii isipokuwa kugoma kutumia simu yao japo kwa siku
moja kuonyesha kutoridhishwa kwangu na uamuzi wao wa kutojali msiba
huu kwa Taifa.

Misiba huweka jamii pamoja. Msiba huu uliotokea Zanzibar ni jaribio
 
kubwa kwa Umoja wa Taifa letu. Shirika la Utangazaji la Taifa
limeshindwa jaribio hili la kudhihirisha Umoja wetu katika kipindi
hiki. Nataraji wakubwa wa Shirika hili linaloendeshwa kwa kodi
watawajibika au kuwajibishwa!

Jumla ya Majeruhi na marehemu sasa inafikia zaidi ya Abiria 800!
 
Asubuhi ya jana 10 Septemba 2011 tuliambiwa na Serikali kwamba uwezo
wa Boti la MV Spice Islander ilikuwa ni abiria 500 na wafanyakazi 12.
Pia tumejulishwa kuwa boti hili lilikuwa la Mizigo na sio la Abiria.

Natumai mara baada ya kumaliza maombolezo haya ya siku tatu Wakuu wa
 
Mamlaka zinazohusika na usafiri wa Majini wa Serikali ya Mapinduzi
Zanzibar watawajibika au kuwajibishwa. Mkuu wa Bandari ya Zanzibar
Mustafa Aboud Jumbe na Waziri wa Miundombinu Hamad Masoud wanapaswa
kufukuzwa kazi mara moja kama hawatawajibika wenyewe kwa kujiuzulu.

Kufukuzwa kwao kazi hakutarudisha ndugu zetu duniani bali itakuwa ni
 
somo kuwa hatutarudia tena kufanya makosa yaliyoleteleza ajali kama
hii.

Mwenyezi Mungu atupe subira wakati huu wa msiba mkubwa katika Taifa
 
letu. Alaze roho za marehemu wetu mahala pema peponi na awape unafuu
wa haraka majeruhi wetu.

Zitto Kabwe, Mb

NAUNGANA NA WATANZANIA WENZANGU KUWAPA POLE WOTE WALIOPATA AJALI NA MELI TOKA UNGUJA-PEMBA

Molla awe pamoja nasi

Wednesday, August 31, 2011

Eid Mubarak

Blog hii inawatakia Eid Mubarak

KIZUNGUMKUTI CHA VITAMBULISHO VYA TAIFA.


Mchakato wa Vitambulisho vya Taifa umeanza tangu mwaka 2007 (kama sikosei). Ni baada ya Baraza la Mawaziri kuubariki Februari 2 mwaka huo. Mwaka 2012 mchakato huu utatimiza miaka mitano. Unagharimu Shilingi bilioni 222! Hiki ni kioja !
Maana; mpaka mradi huu uje ukamilike, basi, yumkini kuna watanzania ambao watakuwa wameshakufa hata bila kuvikamata hivyo vitambulisho vyenyewe. Na pia tujiulize; katika hali yetu ya sasa, mradi wa vitambulisho vya kitaifa unakwamishwa na nini? Kwa hali hii kama wananchi walio wengi wangeambiwa wachague leo, kati ya kitambulisho na nafuu ya bei ya mafuta na sukari, basi, haraka wangechagua kuwepo kwa unafuu wa mafuta na sukari.

Ni tangu enzi za Waziri Joseph Mungai, akaja Lawrence Masha, na sasa Vuai Nahodha. Kila mmoja anakuja na lwake! Bunge la Bajeti 2009 yalisemwa haya na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha:“Naomba kuwathibitishia Watanzania kupitia Bunge lako tukufu kwamba, mradi wa vitambulisho utakamilika kwa kufuata sheria na utaratibu, bila mizengwe, kwa uwazi unaostahili na bila upendeleo,”
Akasimama mbunge wa Kilindi, Beatrice Shelukindo, (CCM) na kusema kwa jazba;“Kama waziri mwenyewe hajui kinachoendelea katika wizara yake ina maana hakuna kinachoendelea. Halafu anatuambia mchakato unaendelea, mchakato gani huo?” aliuliza Shelukindo.
Naibu Spika Anne Makinda akasimama na kutamka: “Mheshimiwa waziri na mheshimiwa mbunge, hapa tunasikilizwa na wananchi nchi nzima. Wanachotaka kujua ni je; vitambulisho watavipata au hawatavipata? Hilo ndilo wanalohitaji na sio kuna nini”.
Waziri Masha akasimama na kusema; ” Mheshimiwa Naibu Spika, vitambulisho vitapatikana ndani ya mwaka huu wa fedha 2009/2010.”
Naam, mpaka hii leo ni August 2011 hakuna cha kitambulisho cha kitaifa wala nini! Waziri Masha alituongopea Watanzania, na hajawahi kutuomba radhi na hayuko tena bungeni. Nani wa kutuomba radhi kwa uongo huu wa serikali ya CCM?????

Serikali iwe wazi kama kuna tatizo la utekelezaji wa mradi wa vitambulisho vya taifa lieleweke ili wadau waweze kutoa maoni mazuri ya uharakishaji wa utekelezaji huo.
Nawasilisha.

Thursday, August 18, 2011

Raha ya SIMBA SC ilipatikana hivi.......

Mafisango akimdhibiti Nsajigwa

Cholo akimdhibiti Tegete

Boban na ball control.....Nsajigwa mmmmh!!!

Victor Costa na Tegete

Cholo akihakikisha Kiiza hapiti

Goooooooooooooooooooooooooooo!!!!!!!!!

Kiduku.....................

Ngao ya Jamii ikikabidhiwa kwa Kaseja wa Simba Sports Club

Thursday, August 11, 2011

HAPPY BIRTHDAY, SOPHY

Salaam na Heri ya maisha marefu.
Natumai kuwa u-mzima na unaendelea vema na harakati za mapambano ya maisha.
Blog hii inakutakia maisha marefu kwa kuonyesha MANENO mazuri, MATENDO safi na MAWAZO thabiti.  Happy birthday  to you!!!




Sunday, August 7, 2011

CHADEMA YATIMUA MADIWANI 5 ARUSHA

CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA).TAARIFA KUHUSU MAAMUZI YA KAMATI KUU YA CHADEMA YALIYOFIKIWA KATIKA MKUTANO WA DHARURA ULIOFANYIKA SIKU YA JUMAMOSI/JUMAPILI TAREHE 06-07 AGOSTI 2011 KATIKA HOTELI YA IMAGI MJINI DODOMA.
Kamati Kuu ya CHADEMA ilikutana katika Mkutano wa Dharura uliofanyika siku ya Jumamosi na Jumapili tarehe 06 Agosti 2011 katika Hoteli ya Imagi Mjini Dodoma. Pamoja na mambo mengine Ilifikia maamuzi yafuatayo :

1. 
Kamati Kuu ilipokea taarifa ya utekelezaji wa maagizo iliyoyatoa katika Mkutano wake wa tarehe 17 Julai 2011 iliyowataka madiwani wa CHADEMA Arusha kujiuzulu nafasi walizozipata pamoja na kuomba radhi kwa makosa waliyoyafanya kutokana na mwafaka uliofikiwa baina yao na madiwani wenzao wa TLP na CCM kwa kuwa chama hakikuridhia wala kuutambua mwafaka huo. 


2. 
Kamati Kuu imezingatia kuwa, kati ya madiwani 10 waliopewa maelekezo na Kamati Kuu, madiwani watano (5) ndio wametekeleza maelekezo kikamilifu wakati madiwani wengine watano (5) wamekataa kuyatekeleza maelekezo hayo.
3. Baada ya kutafakari kwa kina taarifa ya utekelezaji wa maagizo ya Kamati Kuu, na kuwapa nafasi ya kujieleza mbele ya Kamati Kuu Madiwani ambao walikuwa hawajatekeleza maelekezo,Kamati Kuu imezingatia kuwa madiwani wamekataa kutekeleza maagizo ya Kamati Kuu.

Aidha, Kamati Kuu imezingatia kuwa kitendo cha madiwani kukataa kutekeleza maagizo halali ya Kamati Kuu ni utovu mkubwa wa nidhamu na ni kuvunja maadili na kanuni za chama, na kinaenda kinyume na msingi mama wa CHADEMA wa uwajibikaji.

Hivyo basi, kwa kutumia mamlaka ya Kikatiba Kamati Kuu imewafukuza uanachama madiwani watano wafuatao kwa kosa la kukataa kutekeleza maagizo ya Kamati Kuu:


i) 
Ndugu Estomih Mallah


ii) 
Ndugu John Bayo


iii) 
Ndugu Charles Mpanda
iv) Ndugu Rehema Mohamed

v) 
Ndugu Reuben Ngowi
Watajwa hapo juu wamejulishwa maamuzi ya Kamati Kuu ndani ya Mkutano tarehe 07 Agosti 2011 saa 7:57 usiku, Aidha, kila mmoja wao atakabidhiwa barua yenye kueleza maamuzi ya Kamati Kuu.
4. Aidha, Kamati Kuu imepokea taarifa ya mazungumzo baina ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mhe Freeman Mbowe, na Waziri Mkuu, Mhe Mizengo Pinda, juu ya nia na azima ya kumaliza tatizo la mgogoro wa umeya Arusha, waliyoyafanya asubuhi ya siku ya Jumamosi, Tarehe 06 Agosti 2011 nyumbani kwa Waziri Mkuu Mjini Dodoma.

Kamati imezingatia kuwa:
a. Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa na Waziri Mkuu wamekubaliana kuunda Kamati ya Kitaifa ya kushughulikia mgogoro wa umeya wa Arusha itakayojumuisha wajumbe kutoka sehemu mbili zinazohusika katika mgogoro huu ambazo ni CCM na CHADEMA

b. 
Kamati ya Kitaifa ya Maridhiano itaundwa haraka iwezekanavyo, na kwa vyovyote mgogoro wa u meya Manispa ya Arusha ulikubalika uishe ndani ya mwezi mmoja tangu tarehe ya mazungumzo ya Mwenyekiti wa Taifa na Waziri Mkuu


c. 
Uenyekiti wa Kamati ya Kitaifa utakuwa chini ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Ndugu John Tendwa, na kwamba Msajili wa Vyama vya Siasa ataratibu uundwaji wa Kamati hiyo ya Kitaifa.


5. 
Kamati Kuu imetambua juhudi za Waheshimiwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mhe Freeman Mbowe, kwa hatua yao chanya ya kumaliza mgogoro wa Arusha.


6. 
Pamoja na hatua njema kuelekea kumaliza mgogoro wa umeya Arusha, Kamati Kuu ya CHADEMA itaendelea kusitisha kumtambua rasmi Meya wa Arusha hadi pale mazungumzo yaliyoanishwa hapo juu yatakapokamilika na mwafaka bayana kupatikana.
Imetolewa na:……………….Mhe. Freeman Aikaeli Mbowe (Mb)
MWENYEKITI WA TAIFA

Saturday, August 6, 2011

Mpango wa kuinua elimu nchini huu hapa!!!! Wadau mpo???

Mwalimu wa Shule ya Msingi Bungo mkoani Morogoro akisimamia mitihani ya darasa la nne

nani anayemuonea mwenzake HURUMA? je ni anayetoa futari au anayepokea? Check picha.

Hapa mtoto yatima kuna kitu moyoni mwake anajiuliza na kushangaa!!! Lakini mtoaji wa futari wala inaonekana hajali mshangao wa mtoto!! Kuna  jambo zito mtoto analo moyoni. Kuna siku atasema!!!

Friday, July 29, 2011

Msaada tutani....................
















JE ni Heri mbunge atolewe bungeni kwa kutetea nchi yake kama Wenje, Tundu Lisu, Mch Msigwa na Kamanda Lema kuliko mbuge yule anayelala bungeni kama Wassira  huku akisubiri kikao kiishe apokee posho ya 70,000''...????

MAJINA YA SHULE ZETU: ndo utamaduni?


Wednesday, July 27, 2011

Hili haliniingii akilini



















Jamani kuna watu wanapenda kuiga ubunifu wa wenzao. Walianza kuiga kwenye matumizi ya Helcopiter sasa wanaiga matumizi ya MAGWANDA!!! Mwishowe wataiga hata salamu.....utasikia ...Peoples powerrrrrrrrrrr!!!!!!!!!!!!

Tuesday, July 19, 2011

CHADEMA KUMCHUNGUZA SHIBUDA












CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeunda tume itakayoongozwa na Profesa Abdallah Safari kumhoji Mbunge wa Maswa Magharibi, John Shibuda kutokana na tuhuma za utovu wa nidhamu zinazomkabili.

Hii ni mara ya pili kwa Shibuda kuhojiwa na jopo maalumu la Chadema kwani tayari aliwahi kuhojiwa baada ya kupingana na msimamo wa chama hicho wa kumsusia Rais Jakaya Kikwete alipokuwa akizundua Bunge Desemba mwaka jana kwa kuhudhuria dhifa katika Ikulu ya Chamwino huku akiweka bayana kupingana na msimamo huo.

Mapema mwezi huu alitoa tena kauli ambazo Chadema imeziita ni zenye kukiuka maadili hali iliyomfanya Mkurugenzi wake wa Mambo ya Nje, John Mnyika kuwasilisha malalamiko rasmi ndani ya Kamati Kuu (CC).

Akizungumza Dares Salaam jana baada ya kikao cha CC, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa alisema hatua ya kuunda tume kwa ajili kufanya kazi ya kupitia tuhuma hizo imetokana na madai ya mlalamikaji kuwa na mantiki.

Wajumbe wengine wanaounda kamati hiyo ni Edson Mbogoro, Said Mzee, Lazaro Masey na Ester Daffi ambaye si mjumbe wa kamati, bali atafanya kazi kama mratibu wa kamati hiyo akitokea Ofisi ya Katibu Mkuu.

Dk Slaa alisema: “Kikao cha kamati kilichokaa jana (Juzi) hakikujadili suala la Shibuda na mambo yaliyopo bungeni, bali kilipokea taarifa ya malalamiko kutoka Ofisi ya Katibu Mkuu juu ya kitendo cha Shibuda kukiuka maadili. Kwa mujibu wa Katiba ya Chadema ili hatua ziweze kuchukuliwa kwanza ni lazima malalamiko yawasilishwe Ofisi ya Katibu Mkuu wa chama naye kuyawasilisha kwenye Mkutano wa Kamati Kuu.”

MADUDU ALIYOFANYA KATIBU MKUU WA WIZARA YA MADINI NA NISHATI...HATIMAYE AJIUZURU RASMI LEO.

Katibu Mkuu wa wizara hiyo David Jairo (CHINI) amejiuzuru wadhifa wake leo baada ya wabunge kumjia juu kufuatia kitendo chake cha kuziandikia barua taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo zitoe mchango wa sh. milioni 50, ili kufaikisha mchakato wa kusomwa bajeti hiyo bungeni kama barua hiyo inavyosomeka hapo JUU.

Monday, July 18, 2011

WABUNGE WAKATAA UTITIRI WA MIPANGO YA NGEREJA!!!

Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini imekwama kupita na kusogezwa mbele kwa muda wa wiki tatu ili  kutoa majibu muafaka kuhusu mgao wa umeme pamoja na mambo mangine.
Hoja ya kuhairisha bajeti hiyo imetolewa na Kiongozi wa Serikali Bungeni Waziri mkuu Mizengo Pinda, bunge bila kujari itikadi za vyama limepitisha kwa kauli moja hoja hiyo.Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini mwaka 2011/12, ilikuwa mbaya na mbovu isiyofaa hata kupitishwa kwa kutoridhishwa na mipango iliyomo katika bajeti.Miradi 16 iliyohitaji Sh402.4 bilioni ikiwa ni pamoja na matumizi ya kawaida ni:-
1.     Mitambo ya kufua umeme ya megawati 100 jijini Dar es Salaam utakamilika Desemba mwaka huu
2.     Megawati 60 jijini Mwanza ambao utakamilika Juni mwakani.
3.     Kinyerezi (Dar es Salaam) wa megawati 240 (utakamilika mwaka 2013/14),
4.     Mnazi Bay (Mtwara) wa megawati 300 (utakamilika mwaka 2013/14),
5.     Somanga Fungu (Kilwa), megawati 230 (utakamilika mwaka 2013/14)
6.     Ruhudji, megawati 358 (utakamilika mwaka 2015/16).
7.     Mgodi wa makaa ya mawe Kiwira (Mbeya) megawati 200 (utakamilika mwaka 2013/14),
8.     Ngaka wa megawati 400 (utakamilika mwaka 2014/15),
9.     Mchuchuma megawati 600 (utakamilika mwaka 2014/15),
10.  Murongo/Kikagati (Kagerea) wa megawati 16 ambao utategemea kukamilika kwa makubaliano kati ya Serikali ya Uganda na Tanzania.
11.  Rusumo (Kagera) wa megawati 63 ambao upo kwenye taratibu za kutafutiwa fedha,
12.  Stiegler's Gorge (Pwani) wa megawati 2,100
13.  Mpanga wa megawati 165 (utakamilika mwaka 2015/16).
14.  Rumakali wa megawati 222 (utakamilika mwaka 2018),
15.  Dar es Salaam-Tanga ambayo ni ya dharura ikijumuiasha Symbion (megawati 112.5), Aggreko (megawati 100),
16.  Ununuzi wa mitambo itakayofungwa Majani Mapana, Tanga wa megawati 70 na ule wa gesi wa IPTL, Tegeta jijini Dar es Salaam.
Hebu tusubiri watakuja na mipango gani tena baada ya hizo wiki tatu!!!!

Wednesday, July 13, 2011

ROSTAM AJIVUA GAMBA:


HOTUBA YA MHE. ROSTAM AZIZ KWA WAZEE WA IGUNGA - TABORA
UTANGULIZI

WAZEE wangu, kwanza kabisa kabla ya kueleza kile ambacho kimenisukuma kuzungumza nanyi leo, napenda kuanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kutuwezesha kufikia siku hii ambayo inatukutanisha waja wake.

Wazee wangu wa Igunga, baada ya kufanya hivyo napenda pia kutumia fursa hii kuwashukuru ninyi nyote mmoja mmoja na katika umoja wenu kwa kuitikia wito wangu, kijana wenu, niliyewaomba nije nizungumze nanyi siku hii ya leo.

Nafanya hivyo nikitambua vyema kwamba, kama si nyinyi wazee wangu na wengine wengi ambao hatuko nao hapa leo kwa sababu mbalimbali, ambao mmekuwa na imani kubwa nami nisingeweza kufikia hapa nilipofika sasa.

Wazee wangu, waasisi wa taifa letu walitufundisha kutambua na kuheshimu ukweli kwamba; ‘Uongozi ni Dhamana’ dhana ambayo kila ninapokaa na kutafakari huwa inanirejesha nyuma na kukumbuka jinsi nyinyi mlivyokaa katika umoja wenu na kuniteua mimi, miongoni mwa vijana wenu wengi, kuwa mwakilishi wa Jimbo la Igunga tangu mwaka 1994.

Katika kipindi hicho chote cha utumishi wangu, nyinyi wazee wangu mmekuwa mhimili muhimu ambao umeniwezesha kutimiza wajibu wangu kwa bidii kubwa, maarifa na nidhamu ya hali ya juu nikitambua namna ambavyo mmekuwa na imani kubwa juu yangu.

Ari na moyo wa imani, ushirikiano na mshikamano ambao wazee wangu mmekuwa nao kwangu ndiyo ambao kwa kiwango kikubwa umetuwezesha kufanya kazi kwa pamoja, tukishinda changamoto mbalimbali ambazo zimekuwa zikilikabili jimbo letu katika kipindi chote ambacho mmeendelea kuniamini kuwa mbunge wenu kwa miaka 18 sasa.

Wakati nikitambua na kuheshimu ukweli kwamba katika kipindi chote cha ubunge wangu mmekuwa na imani kubwa nami na kuniunga mkono kwa dhati, naamini kwamba kwa upande wangu pia nimejitahidi kwa kadiri nilivyoweza, kutimiza matarajio ya wananchi wa Igunga.

Miongoni mwa mafanikio makubwa tuliyoyafikia kupitia ushirikiano wetu na uongozi wa pamoja ni kwamba, mwaka 1994 Igunga ilikuwa ni wilaya ya mwisho kwa maendeleo mkoani Tabora lakini leo ndiyo ya kwanza, taa za barabarani, bima ya afya kwa kila kaya, zahanati kila kijiji na shule nyingi kuliko idadi ya kata zilizomo kwenye wilaya.

Wazee wangu, nayasema haya nikitambua kwamba, kama ilivyo katika maeneo mbalimbali hapa nchini, mafanikio makubwa tuliyoyapata katika nyanja za elimu, afya, makaazi bora na kilimo katika kipindi chote ambacho mmendelea kuniamini kuwa mbunge wenu kwa miaka 18 sasa.

Wakati nikitambua na kuheshimu ukweli kwamba katika kipindi chote cha ubunge wangu mmekuwa na imani kubwa nami na kuniunga mkono kwa dhati, naamini kwamba kwa upande wangu pia nimejitahidi kwa kadiri nilivyoweza, kutimiza matarajio ya wananchi wa Igunga.

Wazee wangu, nayasema haya nikitambua kwamba, kama ilivyo katika maeneo mbalimbali hapa nchini, mafanikio makubwa tuliyoyapata katika nyanja za elimu, afya, makaazi bora na kilimo katika kipindi hicho chote hayajaweza kumaliza changamoto zote za maendeleo ambazo zinatukabili.

Wazee wangu, ingawa nimekuwa na kawaida ya kukutana na kuzungumza nanyi mara kwa mara, mmoja mmoja na wakati mwingine katika umoja wenu, wito wangu wa leo una makusudi ambayo kwa kiwango kikubwa ni tofauti na yale ambayo tumeyazoea.

Japokuwa ujumbe ninaotaka kuzungumza nanyi wazee wangu, si mgeni sana masikioni mwenu, tofauti ya leo na mikutano yetu mingine iliyopita ni uamuzi ambao nimekusudia kuufanya na ambao nitayatangaza muda mfupi ujao.

YATOKANAYO

Wazee wangu, naamini mmekuwa mkifuatilia kwa karibu hali ya siasa nchini na hususani afya ya kisiasa na matukio mengine ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho mimi ni mwanachama wake na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) nikiuwakilisha Mkoa wetu wa Tabora.

Naamini kwamba katika kufuatilia kwenu mtakuwa mmebaini kuwapo kwa matukio ambayo kwa namna moja au nyingine yamekuwa yakitokea huku yakiligusa jina langu na wakati fulani nafasi yangu kama kiongozi wa chama hicho.

Wazee wangu, nayasema hayo kwa sababu mara kwa mara ninapokutana nanyi nikiwa katika ziara zangu jimboni na wakati mwingine mnapowasiliana nami kwa njia mbalimbali mmekuwa mkionesha kuguswa kushitushwa na kutaka kujua kulikoni kuhusu mambo hayo yanayotokea.

Mimi, kama mnavyonijua nyote, ni mtu muwazi na mkweli. Siku zote nimekuwa mwepesi sana wa kuwaeleza kuhusu kila kinachotokea ili kuwaondoa hofu na wakati huo huo kuwahakikishia kwamba masuala yasiyo na msingi hususani yale yanayogusa siasa za kitaifa hayawezi kutuondoa katika mstari sahihi wa kuwahudumia wananchi wa Igunga, mkiwamo nyinyi wazee wangu ambao mmeniamini na kunituma kuwawakilisha.

Nyinyi wenyewe ni mashahidi wazuri kwamba tangu matukio yanayogusa jina langu yaanze kutokea miezi michache tu baada ya Serikali ya Awamu ya Nne inayoongozwa na Rais Jakaya Kikweti kuingia madarakani kwa mara ya kwanza mwaka 2005, tumekuwa tukiyapuuza na tukaendelea kufanya kazi pamoja kwa bidii.

Bado naamini na nitaendelea kuamini kwamba tulifanya uamuzi sahihi wa kuyapuuza matukio hayo kwani mbali ya kuendelea kutimiza malengo mbalimbali yaliyokuwamo katika Ilani yetu ya Uchaguzi ya CCM, pia mliendelea kuniamini kwa nafasi yangu ya kuwa mwakilishi wenu bungeni na hata mkaniruhusu nibebe jukumu jingine kubwa la kuwa Mjumbe wa NEC ninayewakilisha mkoa wetu wa kihistoria wa Tabora.

Wazee wangu, nyinyi ndiyo watu mnaolifahamu vyema jimbo letu la Igunga na hakika nyinyi ni sehemu muhimu ya watu wanaojua historia ya kisiasa ya Mkoa wa Tabora kwa miaka mingi hata kabla ya kuja kwa mfumo wa vyama vingi hapa nchini.

Hakuna shaka hata kidogo kwamba, Tabora ni kitovu hasa cha uasisi wa siasa za vyama vingi hapa nchini. Ni wazi kwamba huwezi ukazungumzia chimbuko la vyama vya upinzani tunavyoviona hapa nchini leo pasipo kugusa mkoa huu ambao umekuwa chimbuko la wanasiasa wenye mizizi hapa na nchini kwa ujumla.

Majina ya wanasiasa wa aina ya wazee wetu, hayati Chifu Said Abdallah Fundikira na Christopher Kassanga Tumbo, Kasela Bantu (Mungu awalaze mahala pema peponi), James Mapalala, Profesa Ibrahim Lipumba na mengi mengine yana mizizi yao katika Mkoa wetu wa Tabora.

Kutokana na ukweli huo basi ni wazi kwamba, nikiwa Mbunge wa Igunga kwa vipindi vinne mfululizo na wakati huo huo nikiwa Mjumbe wa NEC kwa vipindi vitatu mfululizo, moja ya kazi ambazo nimezifanya kwa uaminifu na kwa bidii kubwa huku nikiungwa mkono na kushirikiana nanyi ni ile ya kuhakikisha kwamba mkoa huu pamoja na kuwa kitovu cha upinzani unaendelea kubakia kuwa ngome muhimu ya kisiasa ya CCM.

Si vibaya tukakumbushana kwamba, wakati nachaguliwa kuwa mjumbe wa NEC wa Mkoa mwaka 1997, jimbo moja katika mkoa wetu lilikuwa likishikiliwa na upinzani. Leo hii Tabora ni mkoa pekee miongoni mwa mikoa iliyotuzunguka ambao haukupoteza jimbo hata moja kwenda upinzani katika Uchaguzi Mkuu wa 2010. Mafanikio haya tuliyafikia kwa pamoja kutokana na ushirikiano wenu wazee wangu.

Wazee wangu, Waswahili wanasema usione vyaelea, vimeundwa. Kazi ya kuijenga CCM katika mazingira yenye mizizi hasa ya upinzani nikiwa mbunge na hususani M-NEC kutoka Mkoa wa Tabora haijapata kuwa rahisi na itaendelea kuwa ngumu na ambayo mapambano yake ni makali sana.

Wazee wangu, kwa namna ya pekee kabisa napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru nyinyi wazee wangu wa Igunga na wananchi wenzangu wote wa Mkoa wa Tabora kwa kushikamana na kuifanya kazi hiyo kwa bidii, uaminifu na mafanikio makubwa.

Matunda ya kazi hiyo kubwa yanaonekana. Pamoja na kuwa kitovu cha kihistoria cha siasa za upinzani, Tabora ndiyo mkoa pekee katika eneo hili ambao unaongozwa na wabunge wote kutoka CCM baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana na hata kabla ya hapo.

Kwa sababu hiyo basi, wazee wangu, sote katika umoja wetu ukiacha mafanikio makubwa tuliyopata katika jimbo na Wilaya yetu ya Igunga, tunayo mambo mengine ya msingi ya kujivunia. Kwa moyo wa dhati na kwa unyenyekevu mkubwa napenda kuwapongeza kwa namna mlivyojitoa kukipigania na kukitetea chama chetu kwa ari na nguvu ya kipekee.

KUJIVUA GAMBA

Wazee wangu, chama chetu chini ya uongozi wa Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete kimeamua kwa kauli na nia moja kujitathmini na kufanya mabadiliko makubwa ya kimfumo yenye lengo la kukiwezesha kiendelee kubakia chama kinachoaminiwa na kuungwa mkono na Watanzania walio wengi.

Dhamira ya mwelekeo huo wa kufanya mabadiliko ya ndani ya chama chetu ilitangazwa rasmi na Mwenyekiti wetu Rais Kikwete wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa kwa CCM, mjini Dodoma.

Katika hotuba yake hiyo, Rais Kikwete aliyafananisha mabadiliko hayo na tabia ya kawaida na ya asili ya nyoka na wanyama wengine kadhaa ya ‘Kujivua Gamba’.

Wazee wangu hatua ya kwanza ya utekelezaji wa azimio hilo na mwelekeo huo sahihi ilifanyika mjini Dodoma wakati wa kikao cha Kamati Kuu ya Taifa ya CCM ambacho mimi nilikuwa mjumbe wake.

Wakati wa kikao hicho, wajumbe wote wa Kamati Kuu na wale wa Sekretarieti ya chama chetu wa wakati huo kwa kauli moja tulikubaliana kujiuzulu, lengo likiwa ni kumpa Mwenyekiti wetu fursa nzuri ya kufanya mabadiliko ya uongozi yatakayotoa nafasi ya kupata mwelekeo mpya wa Chama.

Wazee wangu, tulifanya hivyo tukionesha kuunga mkono kwa asilimia 100 kile ambacho bado naendelea kuamini kuwa ni mawazo sahihi na yenye mwelekeo thabiti ya Mwenyekiti wetu ambayo kwa kiwango kikubwa yalikuwa yakiakisi matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa urais, ubunge na udiwani wa Oktoba mwaka jana.

Niliseme kwa maneno machache tu hili. Ingawa ni kweli kwamba Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana umekirudisha madarakani chama chetu kwa kukipa ushindi mkubwa katika uchaguzi wa urais, ubunge na udiwani kwa Tanzania Bara na Zanzibar, kiwango cha ushindi tulichopata kimeonyesha waziwazi dalili za wananchi kupunguza imani yao kwetu kuilinganisha na ilivyokuwa mwaka 2005.

Tungekuwa ni chama cha siasa cha ovyo iwapo tungepuuza kupungua kwa kura za rais kutoka zaidi ya asilimia 80 tulizopata mwaka 2005 hadi kufikia aislimia 61 mwaka jana kiwango ambacho ni pungufu kwa asilimia 20 ya kura katika kipindi cha miaka mitano tu, hasa ikizingatia ukweli kwamba mgombea urais ni mtu yule yule.

Tungekuwa ni chama cha siasa kilichokosa umakini iwapo tungekaa pasipo kuchukua hatua zozote za kujiimarisha baada ya matokeo ya Uchaguzi Mkuu kuonesha wazi kukua kwa upinzani ambao umeongeza idadi ya wabunge na madiwani katika pande zote mbili za muungano.

Matokeo hayo ya uchaguzi ambayo hapana shaka yamekitikisa chama chetu yalitukumbusha wasia ambao tuliachiwa na Baba wa Taifa aliyesema; ‘Bila ya CCM Madhubuti Nchi Yetu Itayumba’.

Wazee wangu, kwa sababu ya kutambua ukweli kwamba hakuna haki isiyo na wajibu kama nilivyosema awali, mimi na wenzangu tuliokuwa katika Kamati Kuu tuliona ulazima, haja na umuhimu wa kukubali kwa kauli moja wito wa kututaka tujiuzulu ikiwa ni hatua moja ya kujipanga na kukijenga upya chama chetu.

KUJIVUA GAMBA KWAPOTOSHWA

Wazee wangu, kilichotokea baada ya kujiuzulu kwetu kila aliye ndani na nje ya chama chetu amekisikia na anakifahamu. Chama kilipata safu mpya ya uongozi iliyotokana na kuundwa kwa Sekretarieti inayoongozwa na Katibu Mkuu wetu mpya, Mhe. Wilson Mukama, na Kamati Kuu iliyokuwa na sura tofauti na ile ya awali.

Wakati tukitafakari na kuangalia mustakabali mpya wa kisiasa ndani ya chama chetu, ghafla yalianza kutokea mambo ambayo chokochoko zake zilianza kusikika tangu tukiwa ndani ya Kamati Kuu ambayo ilijiuzulu baadaye.

Mara tu baada ya kumalizika kwa kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ambacho kilichagua wajumbe wapya wa Kamati Kuu na kuidhinisha uundwaji wa Sekretarieti mpya, dhana ya kujivua gamba ambayo naamini Mwenyekiti wetu aliianzisha kwa nia njema ilianza kuenezwa ikichukua tafsiri na mwelekeo tofauti na ule wa awali.

Wajumbe wawili wa Sekretarieti, Naibu Katibu Mkuu (Tanzania Bara), Mhe. John Chiligati, na Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi, Mhe. Nape Nnauye, walisikika wakitangaza kwamba Halmashauri Kuu ya Taifa ilikuwa imefikia uamuzi wa kuwapa siku tisini wale walioitwa watuhumiwa wanaokabiliwa na tuhuma za ufisadi ndani ya chama kujitoa katika nafasi zao za uongozi vinginevyo watafukuzwa na chama.

Wazee wangu, baada ya kushinikizwa sana na vyombo vya habari wawataje kwa majina wanasiasa waliokuwa wakituhumiwa kwa ufisadi ambao ni wajumbe wa NEC na ambao wanapaswa kujiuzulu nyadhifa zao, wajumbe hao wa Sekretarieti walikwenda mbele zaidi.

Baada ya awali kuwaeleza waandishi wa habari kwamba majina ya watuhumiwa hao yalikuwa yakifahamika kutokana na kuhusishwa katika kashfa tofauti kama zile za Richmond, EPA na ununuzi wa rada, mwishoni viongozi hao walikaririwa wakiyataja majina ya wanasiasa watatu kuwa ndiyo ambao walikuwa wakilengwa na maamuzi hayo.

Wazee wangu, nilishangazwa na kushitushwa na namna porojo na fitina za kisiasa zilivyofinyangwa kwa mara nyingine tena baada ya kusikia jina la mbunge wenu ambaye ni mimi, likitajwa kuwa miongoni mwa yale matatu ya viongozi waliokuwa wakitakiwa eti kupima wenyewe na kisha kuchukua uamuzi wa kujiuzulu nafasi zao za uongozi ndani ya NEC katika kipindi cha siku tisini.

Niliseme hili mapema. Mshangao na mshituko wangu haukusababishwa na kutajwa kwa jina langu, la hasha, bali namna uamuzi halisi wa NEC na hususani dhana nzima ya ‘kujivua gamba’ ilivyoweza kupindishwa na wajanja wachache na kisha kuendeshwa kwa maslahi binafsi ya kikundi fulani cha watu.

Pili, nilishangazwa na kushitushwa na hatua ya viongozi wa chama changu ambacho nimekitumikia kwa bidii na uaminifu mkubwa kufanya juhudi kubwa hata kukivisha kikao kitukufu cha NEC uamuzi ambao msingi wa hoja zake ni vita vya kimakundi ya kisiasa yaliyo ndani ya CCM kwa upande mmoja na propaganda za vyama vya siasa vya upinzani na vyombo vya habari kwa upande mwingine.

Tatu, nilishangazwa na kushitushwa na ujasiri ambao umekuwa ukioneshwa na baadhi ya viongozi wetu wapya wa Sekretarieti wanaolitaja jina langu na kulihusisha na kile wanachokiita ufisadi ambao hata ukweli wa kimazingira na kihistoria ukiachilia mbali ushahidi wa wazi umeshathibitisha kwamba ni porojo za kisiasa zilizotokana na makovu na matarajio ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 na ule ujao wa 2015.

Wazee wangu, nyinyi ni mashahidi kwamba, mbali ya mimi mwenyewe kujitokeza kupitia vyombo vya habari na kueleza wazi kwamba sijapata kujihusisha katika vitendo vyovyote vya ukiukwaji wa maadili ya uongozi au vya rushwa, hakuna ushahidi wowote uliotolewa unaonihusisha na kashfa yoyote miongoni mwa zile zilizotajwa.

Wazee wangu, ni wazi kwamba kama chama chenye siasa chenye dhamana ya kuwaoongoza Watanzania kutoka katika lindi la ufukara, maradhi, matatizo ya makaazi na mengineyo siku zote tunapaswa kuwa makini katika kuhakikisha kwamba changamoto za kuwaongoza na kuwakomboa wananchi waliotupa dhamana hazitikiswi na mawimbi ya matakwa ya nyakati ama ya vyombo vya habari au wapinzani wetu wa kisiasa walio nje ya CCM.

Ni kwa sababu ya kulitambua hilo na hasa kuyatambua madhara yanayoweza kukipata chama chetu na nchi yetu iwapo tutaendekeza siasa za kupakana matope pasipo na sababu za msingi, kuchafuana kusikokoma na kulipizana kisasi ndiyo maana nimeona nitumie fursa hii kuzungumza nanyi wazee wangu ili kuweka kumbukumbu sahihi.

MAAMUZI YANGU

Wazee wangu, nimetafakari sana na kimsingi nimefikia hatua ya kupima yale ambayo yamekuwa yakisemwa na kuandikwa juu yangu na ambayo kwa mtazamo wangu unaoungwa mkono na wanafamilia yangu, marafiki zangu na washirika wangu wa kibiashara walio ndani na nje ya nchi, naona umefika wakati muafaka wa kuchukua hatua.

Kwa sababu ya kutambua uzito wa hatua ninazokusudia kuzichukua, niliona halitakuwa jambo la hekima hata kidogo iwapo ningefanya hivyo pahala pengine popote bali hapa Igunga mbele ya nyie wazee wangu.

Baada ya kukaa na wanafamilia yangu, marafiki na washirika wangu wa kibiashara niliona halitakuwa jambo la busara hata kidogo kuendelea kuvutana na viongozi wa chama changu na wanachama wenzangu wa CCM katika mambo ambayo yanaweza kumalizwa kwa njia muafaka.

Wazee wangu, sina budi niwaeleze kwamba, mbali ya athari za kisiasa na kifamilia, vita vya ovyo vya kisiasa kama hivi tunavyoviendesha na kuviendeleza ndani ya CCM na ndani ya nchi yetu huwa vina athari kubwa katika ulimwengu wa kibiashara. Athari kama hizo za kibiashara huingia ndani zaidi kuliko vichwa vya habari vya magazeti vinavyolenga kuchafuana, na athari hizo huwa kubwa zaidi kwa mtu kama mimi kwa sababu tofauti na wengine wengi hapa nchini, mimi ni mfanyabiashara wa kimataifa.

Katika ulimwengu wa kibiashara wa leo, vita hivi ambavyo vinaweza kuonekana kuwa ni vidogo tu vyenye malengo ya kuchafuana kisiasa, vinakuwa na athari kubwa katika uhusiano wa kibiashara kuliko hata wale wasioelewa wanavyoweza kukadiria. Ndiyo maana nimeona ni afadhali sasa niwape nafasi wale wanaoendesha siasa hizi uchwara na zisizo na tija waendelee na siasa zao hizo ambazo kwa bahati mbaya kwao, mimi sina muda nazo na siwezi kuwa sehemu yake. Na mimi kwa upande wangu niendelee na maisha yangu.

Kutokana na ukweli huo na sababu zote hizo basi, kwa moyo wa dhati na kwa nia thabiti, hatua ya kwanza niliyoiona kuwa ninapaswa kuichukua ilikuwa ni hii ya kuitikia wito unaotokana na msukumo wa ndani ya nafsi yangu wa kuamua kukomesha kabisa malumbano na mivutano isiyo na manufaa kwangu binafsi, kwa viongozi wa chama changu na chama chenyewe.

Msukumo huo si mwingine bali ni ule wa kuamua kuachia nafasi zangu zote za uongozi ndani ya chama, nikianzia na ile ya ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa nikiuwakilisha Mkoa wa Tabora na hii ya ubunge wa Igunga ambazo kama si kwa baraka za chama changu nisingelikuwa nazo.

Napenda kuliweka hili sawa sawa. Uamuzi wangu wa kuachia nafasi zangu zote za uongozi nilizopata kwa tiketi ya CCM haukutokana na wala haumaanishi kukubaliana na shinikizo lililopotoshwa kuhusu azma ya utekelezaji wa dhana ya kujivua gamba, la hasha, bali dhamira ya dhati ya kuachana na siasa hizi uchwara (gutter politics) na kutumia muda wangu kushughulika na biashara zangu.

Aidha, nimefikia uamuzi huo lengo likiwa ni kuwajengea heshima na imani machoni mwa wanachama na wananchi wengine, viongozi wangu ambao naamini baada ya mimi kujitoa watapata fursa ya kutafakari upya changamoto nyingine mbadala zinazowakabili ambazo msingi wake ni dhamana kubwa walizo nazo za kukiongoza chama chetu na nchi yetu kupitia Serikali yake.

Wakati nachukua uamuzi huu, natambua vyema kwamba, watatokea watu ndani ya chama chetu na nje ambao watafanya kila juhudi kupotosha au kupindisha ukweli kuhusu hatima yangu ya kisiasa baada ya kujiweka kando na kujipa mimi mwenyewe na chama changu fursa ya kutafakari kwa kina majaaliwa yangu na ya nchi yangu katika siku zijazo.

Nafanya hivyo nikiwa na imani thabiti kwamba, uamuzi wangu huu, hususani ule wa kuachia nafasi yangu ya ubunge, yatakipa fursa nyingine CCM ya kuendelea kuliongoza jimbo letu la Igunga katika kipindi cha miaka minne ijayo kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Kwa upande mwingine, uamuzi wangu huu naona ni fursa kwa viongozi wa Chama changu cha CCM kutafakari na kuamua njia wanayoiona wao ni sahihi kuichukua kwa hatima na mustakabali wa chama chetu na ambayo wanaamini itakipa nguvu mpya ya kisiasa dhidi ya vyama vya upinzani.

Sambamba na hilo, ninayo imani thabiti kwamba, uamuzi wangu wa kubakia kuwa mwanachama wa kawaida na mtiifu wa CCM utakuwa chachu kwa chama changu na kwa Serikali yake kuwatumikia wananchi kwa Ari Zaidi, Kasi Zaidi na Nguvu Zaidi.

Mwisho kabisa, nikimalizia naomba nitumie fursa hii kutoa heshima za pekee kwa Rais Jakaya Kikwete kwa kazi kubwa aliyoifanyia na anayoendelea kuifanyia nchi yetu. Amefanya mengi na makubwa kuiendeleza nchi yetu na watu wake kuliko inavyothaminiwa na kufahamika. Kazi yake kubwa inashindwa kuthaminiwa na kufahamika kutokana na siasa chafu tunazoziendesha Tanzania. Wasia wangu kwa wanasiasa wenzangu, waandishi wa habari na Watanzania wenzangu kwa ujumla ni kuwa tunahitaji kuisaidia nchi yetu kwa kufanya siasa zenye mwelekeo wa kujenga ambazo ndiyo hasa zinapaswa kuwa siasa kwa maana halisi ya neno hilo.

Wazee wangu, baada ya maelezo hayo, nawashukuru sana kwa kunisikiliza na kunielewa.

Ahsanteni sana.

Mwisho…