Search This Blog

Thursday, September 15, 2011

Miaka 50 ya Uhuru: UKWELI NA UONGO!


Hivi ni kweli kabisa kuwa 09/12/2011 tunasherehekea miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania??Sasa hivi kila idara ya serikali, mashirika na taasisi zake zinafanya maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru.
Hebu tutafakari kwa akili huru kwa pamoja
1. Tanzania ilizaliwa mara baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kuungana tarehe 26/04/1964 ambako mpaka leo ni miaka 47 ya muungano kwa maana hiyo Tanzania ina miaka 47 na sio 50 kama tunavyorubuniwa nah ii serikali na kutumia fedha nyingi kutangaza eti miaka 50 ya uhuru wa Tanzania
2. Kwanini Serikali isiseme tunasherehekea miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika au Tanzania Bara badala ya kuendelea kusema Tanzania?? Na kama dhana ni miaka 50 ya uhuru basi ni UHURU wa TANGANYIKA na siyo Tanzania.
3. Siku ya sherehe ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania kama wanavyosema wimbo gani wa Taifa utaimbwa?Mungu Ibariki ambao ni wimbo wa taifa Tanganyika na Zanzibar kwa Ujumla au utaimbwa uliokuwa wimbo wa Tanganyika? Au ule wa wasanii wa bongoflava??
4. Siku ya sherehe bendera gani itapeperushwa na kupandishwa?hii inayotumika sasa ikiashiria Muungano wa Tanganyika na Zanzibar au ile ya Tanganyika ambayo daima mzee  Mtikila huipandisha?
5. Mgeni Rasmi atakuwa nani?Mhe Jakaya Kikwete ambae ni Rais wa jumla wa Tanzania bara na Zanzibar?
Imefika wakati wa kuwa na Bendera ya Tanganyika kama ilivyo Zanzibar, Jina la Tanganyika likaendelea kuwepo na kutambulika kama lilivyo la Zanzibar, Heri tukawa na Wimbo wa Taifa la Tanganyika kama ilivyokuwa zanzibar
Mbona Zanzibar wakisherehekea miaka yao mapinduzi huwa wanapandisha bendera yao?mbona wao wana imba nyimbo za kusifu mapinduzi na wimbo wa taifa lao?
Nawasilisha!!!!!!!



No comments:

Post a Comment