Search This Blog

Thursday, January 6, 2011

KIKWETE KUHUDHURIA MAZISHI YA WAIOUAWA ARUSHA????

Inasemekana watu takribani kumi (10) wameuawa katika maandamano yaliyofanyika jana terehe 5/1/2011 Arusha. Katika maandamano hayo ambayo inasemekana CHADEMA walikuwa na barua ya kuwaruhusu toka kwa Msajili wa vyama vya siasa ambaye aribariki maandamano hayo. hata hivyo kisheria IGP alitakiwa aandikie barua CHADEMA kubatilisha ile ya awali then wangeandamana ingekuwa ukaidi. 


Demokrasia ni ghali na ina gharama yake, HAKI SAWA KWA WOTE, Vyama vya Siasa vimeandikishwa kisheria na vina wanachama waadilifu , Na ni hiari yao kuwa wanakutana bila kuvunja sheria. Ni kosa wanapoonewa bila sababu ya Msingi.Huwezi kuwazuia kuandamana kama wana kibali, hii ni kuleta Siasa za CHUKI, CHUKI Haina Nafasi.


Kitendo cha polisi kujiingiza katika siasa na kukataza mara kwa mara mikutano na maandamano ya Chadema, ni moja ya ukiukwaji wa haki za binadamu.Polisi wamemwaga damu, wamekamata hadi wabunge akiwemo kiongozi wa upinzani bungeni (Freeman Mbowe).


JE, Kikwete atahudhulia mazishi ya hawa wapendwa wetu waliouawa Arusha na Polisi wake?????.

No comments:

Post a Comment