Search This Blog

Sunday, January 23, 2011

CHADEMA NA MCHAKATO WA KATIBA MPYA: Mkutano wa hadhara DSM

Katibu Mkuu Dr. Slaa akisalimiana na wananchi

 Mwanzilishi wa Mageuzi Nchini Tanzania Mabere Marando ambaye kwa sasa ni mwanachama wa Chadema akiwasalimia mamia ya wananchini waliofurika kwenye mkutano wa hadhara viwanja vya mtaa wa mwongozo Makuburi-Mabibo  Dar es Salaam
 Mbunge wa Kigoma Kaskazini ambaye pia ni naibu katibu mkuu wa chadema Zitto Kabwe akimwaga cheche kwenye mkutano huo na ulioudhuriwa na wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali mbalimbali na Mamia ya  wananchi
 Wananchi wakirudisha kadi za CCM na kujiunga CHADEMA
 Sehemu ya umati wa watu
"Narudisha kadi ya CCM najiunga CHADEMA leo"

Friday, January 21, 2011

MIKIKI MIKIKI!!!!!!!!!! NINAWATAKIA WIKENDI NJEMA!!!!!!!

IKO WAPI INTELIJENSIA YA POLISI??


MFUMO wa Polisi, vyombo vingine vya ulinzi na usalama na serikali,wa kukusanyia na kusafirishia taarifa, hasa za “usalama,” ujulikanao kama intelijensia una walakini.
Said Mwema, inspekta jenerali wa polisi (IGP), alisema alikuwa na “taarifa za kiintelijensia” kuwa kutatokea vurugu iwapo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kitafanya maandamano mjini Arusha.
Iko wapi intelijensia ya polisi isiyoweza kuona Mafisadi na kuwakamata wanaounda makampuni na kuiba mabilioni ya shilingi kutoka Benki Kuu na Hazina?
Iko wapi Intelijensia ya IGP Mwema isiyoweza kujua mmiliki wa Dowans na ndugu yake Richmond? Kwa nini inteligensia ya Mwema isizuie malipo ya mabilioni ya shilingi kufidia kisichoeleweka wakati wahusika wapo?
Au hii Intelijensia ni kwa Chadema tu????????????????

Friday, January 7, 2011

CCM NA UNYANYASAJI WA KIJINSIA


Josephine Mushumbushi.

Matumizi ya nguvu yaliyofanywa na Serikali ya CCM mjini Arusha yamedhihilisha unyanyasi wa kijinsia wa hali ya juu sana. Pichani anaonekana mwanamke (Mchumba wa Dr. Slaa) aliyepigwa sana na Polisi hadi kupasuka kichwa na kuvuja damu kama anavyoonekana. Hebu iangalie picha kwa umakini uone ni kiasi gani cha damu iliyomwagika. 
Sidhani kama kweli akina mama wa aina hii hapa Tanzania wanaweza kuwa na vurugu hadi kusababisha askari kuwapiga kwa kutumia silaha za moto. Wanawake wengi walianguka mitaroni, kupigwa na risasi za moto, kupigwa mabomu ya machozi,  kumwagiwa maji ya pilipili ikiwa ni kuwadhalilisha na kuwanyanyasa. Baada ya kujeruhiwa vibaya, Mushumbushi na wanawake wengine walienda Polisi kuchukua PF3 kama haki ya kila mtanzania - matokeo yake wakawekwa rumande na kuendelea kuteseka kwa maumivu makali. 
Mhe.Lucy Owenya baada ya kipigo alizirai na kuokolewa na wananchi ambao walikuwa wanakimbia kuokoa roho zao. Gari la Mbunge wa Viti maalumu Mjini Moshi, Mhe Grace Kihweru liliharibiwa na Askari. Akina mama waliokuwepo kwenye maandamao hawakuwa na silaha za kuwatishia polisi. Kitendo cha polisi kutumia nguvu kubwa kupita kiasi ni ukiukwaji wa haki za binadamu na kinasikitisha.

Blog hii inawapa pole wanawake wote walioathirika na ukatiri wa serikali ya CCM.

Thursday, January 6, 2011

KAMA TULIVYOTARAJIA NA WENGI: CHADEMA YACHUKUA UMEYA, NA UNAIBU MEYA JIJI LA MWANZA.

 Hatimaye jiji la Mwanza leo limepata Meya wake mpya baada ya kura za Madiwani wapatao 32 kupigwa nazo kuhesabiwa na hatimaye diwani wa kata ya Nyakato bw. Josephat Manyerere wa CHADEMA kutangazwa kuwa ndiye meya mpya wa jiji la Mwanza.

Akitangaza matokeo ya umeya Mwanza, msimamizi wa uchaguzi huo ambaye ni mkurugenzi wa jiji bw. Wilson Kabwe amemtaja Bw. Stanslaus Mabula (CCM) kuwa amepata kura 15, na Bw. Josephat Manyerere (CHADEMA) akiibuka mshindi kwa kupata kura 17.
Mjengoni jiji la Mwanza
Huyu ndiye meya mpya wa jiji la Mwanza kupitia CHADEMA Bw.Josephat Manyerere(kulia) akipongezwa na mbunge wa Nyamagana Mh.Wenje, na kwa chati pembeni ni diwani wa Mwaloni Kirumba Bw.Novat Manoko.


Mhe. Wenje akipongezana na Mhe. Zito Kabwe

Mara baada ya mchakato wa kumpata Meya kumalizika na mshindi kutajwa, ungwe iliyofuata ikawa ni kumsaka Naibu Meya ambapo kulikuwa na wagombea wawili nayo matokeo yakataja kuwa diwani Charles Marwa Chichibela (pichani mwenye suti) kutoka CHADEMA ameibuka kidedea kwa kuzinyakua kura 17, dhidi ya 15 za Daudi Mkama wa CUF.

KIKWETE KUHUDHURIA MAZISHI YA WAIOUAWA ARUSHA????

Inasemekana watu takribani kumi (10) wameuawa katika maandamano yaliyofanyika jana terehe 5/1/2011 Arusha. Katika maandamano hayo ambayo inasemekana CHADEMA walikuwa na barua ya kuwaruhusu toka kwa Msajili wa vyama vya siasa ambaye aribariki maandamano hayo. hata hivyo kisheria IGP alitakiwa aandikie barua CHADEMA kubatilisha ile ya awali then wangeandamana ingekuwa ukaidi. 


Demokrasia ni ghali na ina gharama yake, HAKI SAWA KWA WOTE, Vyama vya Siasa vimeandikishwa kisheria na vina wanachama waadilifu , Na ni hiari yao kuwa wanakutana bila kuvunja sheria. Ni kosa wanapoonewa bila sababu ya Msingi.Huwezi kuwazuia kuandamana kama wana kibali, hii ni kuleta Siasa za CHUKI, CHUKI Haina Nafasi.


Kitendo cha polisi kujiingiza katika siasa na kukataza mara kwa mara mikutano na maandamano ya Chadema, ni moja ya ukiukwaji wa haki za binadamu.Polisi wamemwaga damu, wamekamata hadi wabunge akiwemo kiongozi wa upinzani bungeni (Freeman Mbowe).


JE, Kikwete atahudhulia mazishi ya hawa wapendwa wetu waliouawa Arusha na Polisi wake?????.

VIONGOZI WA CHADEMA WAKAMATWA KUTOKANA NA MAANDAMANO ARUSHA

Viongozi wa CHADEMA

Polisi wakizuia maandamano
Maeneo ya Unga Limited palikuwa hapatoshi

MWENYEKITI WA CHADEMA NA MBUNGE WA HAI MH. FREEMAN MBOWE NI MIONGONI MWA VIONGOZI KADHAA WA CHAMA HICHO AMBAO WAKO MIKONONI MWA POLISI JIJINI ARUSHA DAKIKA HII, BAADA YA KUTIWA MBARONI KWA KILE KILICHOONEKANA KUWA MAANDAMANO BATILI.

VIONGOZI WENGINE WALIO KOROKORONI KUWA NI MBUNGE WA ARUSHA MJINI MH. GODBLESS LEMA, MBUNGE WA ROMBO MH. JOSEPH SELASINI NA WANACHAMA WENGINE KADHAA WA CHADEMA.

HABARI ZINASEMA POLISI WALITAWANYA MAANDAMANO HAYO YALIPOKARIBIA OFISI ZA TAKUKURU NA KWAMBA BAADA YA VUTA NIKUVUTE, MH. MBOWE NA WENZIE WAKAKAMATWA NA KUTUPWA RUMANDE.

AIDHA HABARI ZINADATISHA KWAMBA JIJI LA ARUSHA LINARINDIMA KWA MPAMBANO WA KUKIMBIZANA WA POLISI NA MAKUNDI YA WATU WANAODAIWA KUTAKA KWENDA KITUO CHA POLISI KUWATOA WALIOKAMATWA KWA NGUVU.

Kabla ya kukamatwa.............

Mh. Freeman Mbowe akizungumza na Tanzania Daima kutoka Arusha jana jioni alisema maandamano hayo yatakayohitimishwa na mkutano mkubwa wa hadhara, ajenda yake kuu ni kupinga hatua ya serikali kuvunja sheria kwa makusudi na kukipa Chama cha Mapinduzi (CCM) ushindi ulio kinyume cha sheria katika uchaguzi wa umeya uliofanyika hivi karibuni.

Mbowe akizungumza na Tanzania Daima kutoka jijini Arusha jana jioni alisema CHADEMA itaanza rasmi kuitumia nguvu ya umma kupinga kile alichokiita "uhuni uliofanywa na CCM na serikali yake kujipa ushindi wa lazima katika uchaguzi wa umeya kinyume na matakwa ya sheria halali za nchi.

"Mwanza hakujafanyika uchaguzi kwa sababu ya dhuluma, Kigoma na Arusha uchaguzi ulikuwa batili kabisa. Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI) tumemsihi sana aingilie kati lakini ameendelea kushirikiana na chama chake (CCM) kuinyima CHADEMA haki ya kuongoza. Tunakwenda kulaani kwa nguvu zote uchakachuaji wa maamuzi ya wananchi" alisema Mbowe.