Search This Blog

Monday, March 7, 2011

SERIKALI YA CCM INAVYOCHEMKA...Mhe Pinda Kamkataza Mgufuri kubomoa nyumba



WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, amemwagiza Waziri wa Ujenzi, Dk.John Magufuli, kusitisha mara moja operesheni bomoabomoa inayoendelea nchini hadi serikali itakapotafakari upya suala hilo. Alitoa agizo hilo jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Chato, mkoani Kagera.
Waziri Mkuu alisema uamuzi huo unatokana na malalamiko mengi yanayotolewa na wananchi ikiwemo kutopewa elimu ya kutosha juu ya operesheni hiyo.
"Magufuli akishaagiza, meneja wa TANROADS jasho linamtoka na kuanza kubomoa... hatuendi hivyo. Ukitizama X wanalolibandika linakera," alisema Waziri Mkuu.

Hii serikali bwana!!!!!!!!!! . Maagizo yanatolewa barabarani. Kwanini asimuite ofisini kwake akampa maagizo ya kusitisha zoezi hilo? Halafu amwachie yeye mwenyewe atangaze?
Hapo Magufuli kesha vunjwa moyo na kwa kifupi amedhalilishwa mbele ya Tanroads na mbele ya wapiga kura wake na mbele ya watanzania kwa ujumla. Unadhani hata mbeleni atakapotoa maagizo, si wananchi  watamwambia subiri kwanza Waziri Mkuu akubali. Hii ndiyo CCM bana!!!!

Hii tabia ya kila kiongozi wa serikali kutoa tamko namna anavyoona yeye tena vikao vya barabarani inaonyesha kuwa kuna tatizo kubwa la uongozi (leadership) kwenye serikali kwa sasa.

Kibaya zaidi ili tatizo litaigharimu sana nchi na wananchi wake kwa sababu kila kiongozi atafanya lile ambalo anaona linafaa kwake yeye binafsi na hii ni hasara kubwa kwa taifa.

Leadership ni kitu muhimu sana mahali popote pale panapokuwa na watu au viumbe zaidi wa mmoja. Hata wanyama, wadudu, ndege wa angani, samaki wa baharini wana kiongozi wao na wanafuata kila kile kiongozi anacho fanya. Kiongozi si jina tu bali ni matendo. Kiongozi lazima kweli aonekane ni kiongozi na wale wanafuata watambue kuwa kuna kiongozi na watufuate njia zake.

Hii tabia ya viongozi wa serikali tena Mawaziri kila mmoja kuja na kauli tofauti kwenye jambo moja kwa kweli inakera na kuchanganya sana wananchi.
HATUDANGANYIKI!!!!!!!!!!!!!

No comments:

Post a Comment