Search This Blog

Tuesday, December 14, 2010

ASERNAL HOI KWA MASHETANI WEKUNDU

JI-SUNG PARK.Bao safi kwa kichwa la Ji-Sung Park katika kipindi cha kwanza, lilitosha kuipatia ushindi Manchester United dhidi ya Arsenal na kuwawezesha kushikilia usukani wa ligi kutoka kwa mahasimu wao hao.

Nafasi nzuri kwa Arsenal ilikuwa ni ya Marouane Chamakh, ambaye alikosa kufunga baada ya mpira wa kichwa alioupiga kuzuiwa na Nemanja Vidic.

WAYNE ROONEY.Wayne Rooney angeweza kuongeza bao la pili, lakini mkwaju wake wa penalti baada ya Clichy kuunawa mpira, ukapaa juu ya lango la Arsenal.
Kwa matokeo hayo, Manchester United sasa wamefikisha pointi 34 wakiwa na mchezo mmoja mkononi, wakifuatiwa na Arsenal yenye pointi 32, sawa na Manchester City iliyo nafasi ya tatu na Chelsea watakaopambana na Manchester United siku ya Jumapili ijayo wapo nafasi ya nne na pointi 31.

No comments:

Post a Comment